
“Uamuzi uliochukuliwa na Uingereza utaathiri Kenya kwa kiasi kikubwa hasa kibiashara kati ya Kenya na Uingereza, usafiri, utalii na ushirikiano wa kiusalama,” Wizara ilisema.
Pia wizara ya Kenya ilisistiza kuwa hatua ya uamuzi huo utatatiza shughuli za nchi hizo mbili hasa ikizingatiwa kwamba zimekuwa na ushirikiano wa nyanja mbalimbali kama vile afya, elimu na hata baina ya watu.
“Zaidi, uamuzi huo wa upande mmoja haukuakisi mantiki na ufahamu wa kisayansi kuhusu ugonjwa huo au kusambaa kwa janga. Badala yake unaonekana kuchochewa na sera ya kubaguzi dhidi ya mataifa mengine na watu wake”.
Serikali ya Kenya pia ilizungumzia kusikitishwa na kile ilicho kiita ubaguzi wa chanjo ambapo nchi zinazotengeneza chanjo sasa zinabagua nchi zingine na kuamua kijiwekea akiba.
“Kenya bado imesalia na maoni yake kwamba serikali ya Uingereza ingeiunga mkono kwa kuipatia chanjo. Hii ni baada ya Kenya kuiomba Uingereza kuigawanya chanjo zake ambayo inafahamu kwamba ina idadi kubwa kuliko zile inazotumia kwa sasa”.
Wizara ya mambo ya nje iliongeza kuwa wimbi la tatu la maambukizi ambalo Kenya inakabiliana nalo sasa hivi na hatua ilizochukua, ni mfano vile Wakenya walivyojitolea kuhakikisha ugonjwa wa corona hausambai ama nchini Kenya au kwingineko duniani.
Pia Kenya imezungumzia ufahamu kwa kwamba chimbuko la ugonjwa huo sio Afrika, hauna mipaka na wala haujakuwepo kwa muda mrefu kwa mwanadamu kuweza kuelewa mabadiliko ya siku za usoni.
Post a Comment